Hatua za Kufuatilia Cheti Kilichopotea

C By Captain
May 1, 2025
Hatua za Kufuatilia Cheti Kilichopotea

Andika Taarifa ya Kupoteza (Loss Report) Polisi

  • Nenda kituo cha polisi chochote.

  • Eleza kuwa umepoteza cheti chako.

  • Utapewa RB (Report Book) number au loss report kama uthibitisho rasmi.

2. Weka Tangazo la Kupotea kwenye Gazeti

  • Chapisha tangazo fupi kwenye gazeti la kitaifa (mfano: Mwananchi, HabariLeo).

  • Eleza jina lako kamili, aina ya cheti, mwaka wa kuhitimu, na kwamba kimepotea.

3. Andaa Barua ya Maombi ya Nakala Mbadala

  • Iandikwe kwenda kwa Katibu Mtendaji wa Baraza husika (NECTA au NACTE au TCU).

  • Taja jina lako, namba ya mtihani, shule na mwaka uliomaliza.

  • Eleza kuwa umepoteza cheti na unaomba duplicate.

4. Ambatanisha na Barua:

  • Nakala ya tangazo la gazeti.

  • RB (loss report) kutoka polisi.

  • Kitambulisho chako (NIDA au kura).

  • Passport size moja au mbili.

  • Malipo ya ada ya duplicate certificate (kwa NECTA ni TZS 20,000).

5. Wasilisha kwa Baraza Husika:

  • Kama ni NECTA: Wapelekee makao makuu (Dar es Salaam) au ofisi za NECTA za kanda.

  • Kama ni NACTE/TCU kwa vyuo: Wasiliana na chuo husika pia kwa uthibitisho wa kwanza.

6. Subiri Majibu

  • NECTA huchukua wiki kadhaa hadi miezi 2.

  • Watakupa nakala halali (official copy) ya cheti chako.

 

Chat with us!
Home Blog Talents Cart Search